NSSF SINGIDA WAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUCHANGIA DAMU - FAHARI NEWS

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Saturday, October 8, 2022

demo-image

NSSF SINGIDA WAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUCHANGIA DAMU

Responsive Ads Here

1
Wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Singida pamoja na wanachama wa mfuko huo, wakiongozwa na Meneja wa NSSF mkoani humo, Oscar Kalimilwa (katikati) kushika keki ikiwa ni moja la matukio katika kilele cha     Maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja yaliyofanyika jana.2Muonekano wa keki hiyo.
Capture
Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida , Oscar Kalimilwa akizungumza kwenye maadhimisho hayo.
Capture.PNG1
Afisa Huduma kwa Wateja NSSF Mkoa wa Singida, Latifa Singano akizungumza.
Capture.PNG2
Mhasibu wa NSSF Mkoa wa Singida, Keneth Kalinjumani, akizungumza.
Capture.PNG3
Afisa Ustawi wa Jamii Hospitali ya Mkoa wa Singida, Lucretia Mseli akizungumza wakati akipokea msaada wa vitu mbalimbali kutoka NSSF kwa niaba ya Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo.
DSC_2985
Wafanyakazi Wanawake wa NSSF Mkoa wa Singida wakiwa katika picha ya pamoja.
DSC_3017
Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida , Oscar Kalimilwa akimlisha keki mmoja wa wanachama wao, Christina Maro.
DSC_3020
Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida , Oscar Kalimilwa akimlisha keki mmoja wa wanachama wao, Bahati Masalago.DSC_3021Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida , Oscar Kalimilwa akimlisha keki mmoja wa wanachama wao, Saumu Sadiki kutoka Mwenge Manispaa ya Singida.
DSC_3023
Zoezi la kulishana keki likiendelea.
DSC_3035
Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida , Oscar Kalimilwa akimlisha keki, Afisa Huduma kwa Wateja, Latifa Singano..
DSC_3047
Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida , Oscar Kalimilwa (kulia) akimlisha keki Afisa Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Singida, Donald Lembeli. 
DSC_3056
Picha ya pamoja.
DSC_3059
Picha ya pamoja,wageni waalikwa na wanachama wa NSSF.DSC_3071
Wafanyakazi Wanawake wa NSSF Mkoa wa Singida wakiwa katika picha ya pamoja.
DSC_3094
Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida , Oscar Kalimilwa akimlisha, akisaini kitabu cha wageni wakati wa kukabidhi msaada Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida Mandewa.
DSC_3101
Afisa Utawala wa NSSF Mkoa wa Singida, Christian Magwila akizungumza wakati wa kutoa msaada huo.
DSC_3118
Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida , Oscar Kalimilwa akimkabidhi msaada huo Muuguzi wa zamu wa Hospitali hiyo, Amina Thomas.
DSC_3128
Wafanyakazi wa NSSF Mkoa wa Singida wakiwa na vitu mbalimbali walivyotoa msaada Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida.
DSC_3161
Katibu Muhtasi Ofisi ya Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida, Asha Kiwamba akiwajibika wakati wa maadhimisho hayo.
IMG-20221008-WA0025
Wafanyakazi wa NSSF wakichangia damu kitengo cha damu salama Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida.
IMG-20221008-WA0035
Uchangiaji damu ukiendelea.
.......................................................

Dotto Mwaibale na Philemon Solomon, Singida

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Singida umeadhimisha wiki ya huduma kwa wateja kwa kutoa msaada wa damu, sabuni, mashuka, pampasi mafuta ya kupaka, nguo za watoto, dawa za meno na miswaki katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Meneja wa NSSF Mkoa wa Singida, Oscar Kalimilwa alisema wametoa msaada huo kwa jamii kuonesha kuwajali wateja wao na wananchi chini ya kauli mbiu isemayo ‘Huduma bora ndio kipaumbele chetu’

Alisema mbali na kutoa msaada huo waliandaa keki maalumu walioila pamoja na wateja wao ikiwa ni ishara ya kuwathamini kwani ndio wanaowafanya waendelee kuwepo

Aidha Kalimilwa alisema walitumia siku hiyo kutoa elimu kwa wanachama ambao hawana elimu kuhusu mifuko huo wa jamii ambao ni muhimu sana na kutoa wito kwa waajiri kuendelea kutoa michango ya wanachama wao ili wanapokutana na majanga ambayo NSSF inashughulika nayo kuwahudumia iweze kuwasaidia kwa kutoa huduma bora kama kauli mbiu yao inavyosema.

Mhasibu wa NSSF Mkoa wa Singida, Keneth Kalinjumani aliwapongeza wanachama wote walioamua kujiunga NSSF kwani hawezi kujuta kwani mfuko huo unatoa huduma bora na hawatajuta katika maisha yao.

Alisema NSSF inafanya vitu vingi vya kuwasaidia wanachama wao vya kuwakinga na majanga na akawahimiza waajiri kutosita kuwapeleka waajiriwa waokuwaandikisha katika mfuko huo kwani watakuwa wakiwawekea mazingira mazuri baada ya kustaafu utumishi wao.

Afisa Huduma kwa Wateja Latifa Singano aliwahimiza wananchi kujiunga katika mfuko huo ili waweze kuwahudumia kwani ndio jukumu lao.

Afisa Ustawi wa Jamii Hospitali ya Mkoa wa Singida, Lucretia Mseli akipokea msaada huo kwa niaba ya Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo aliwashukuru NSSF kwa kutoa faraja kwa watu wenye uhitaji waliopo hospitalini hapo ambapo alitoaa wito kwa wadau wengine na mtu mmoja na taasisi waguswe kwa kutembelea katika zahanati, hospitali na vituo vya afya kuwaona wagonjwa wenye uhitaji na kuwasaidia.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages

undefined

Contact Form

Name

Email *

Message *