WAZIRI BASHE AGEUKA MBOGO BAADA YA MBOLEA KUTOPELEKWA KWA WAKULIMA SINGIDA - FAHARI NEWS

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Wednesday, October 5, 2022

demo-image

WAZIRI BASHE AGEUKA MBOGO BAADA YA MBOLEA KUTOPELEKWA KWA WAKULIMA SINGIDA

Responsive Ads Here

DSC_2957
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida, Jeshi Lupembe (kulia) akionesha mmoja wa mfuko wenye mbegu za  alizeti baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (katikati) wakati wa hafla ya kuzizindua iliyoongozwa na Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe iliyofanyika Oktoba 5,2022 mkoani Singida.
DSC_2916
Balozi wa Pamba Nchini, Aggrey Mwanri akizungumza kwenye uzinduzi huo.
1
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mbegu hizo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba na kushoto ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Juma Killimbah.
2
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, akimkabidhi mbegu hizo Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba. 
5
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe (kulia) akipata maelezo alipotembelea kukagua banda la mbolea.
DSC_2958
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba akimkabidhi mbegu hizo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Ester Chaula.
DSC_2964
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Dk. Stephen Ngailo akimkabidhi mbolea Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Singida, Ahmed Kaburu baada ya kuinunua kwa mfumo wa kimtandao uliozinduliwa na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe wakati wa hafla hiyo. Kulia ni Meneja wa TFRA Kanda ya Kati, Joshua Ng'onya.
DSC_9360
Ukaguzi wa mabanda ukiendelea.
DSC_9427
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mauzo wa Kiwanda cha Singida Fresh Oil Mill, Jamal Shabani alipotembelea kukagua banda la kiwanda hicho.
DSC_9532
Taswira ya meza kuu katika uzinduzihuo.
DSC_9519
Uzinduzi ukiendelea.
DSC_9515
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye hafla hiyo.

DSC_2919
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Dk.Godfrey Mkamilo akizungumza katika hafla hiyo.
DSC_9534
Mtendaji  Mkuu wa Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA), Dk. Sophia Kashenge, akitoa taarifa kuhusu mbegu hizo.
.........................................

Dotto Mwaibale na Philemon Solomon, Singida 

WAZIRI wa Kilimo Hussein Bashe amekuwa mbogo baada ya kusikia mbolea bado hazijaanza kusambazwa kwa wakulima mkoani hapa licha ya msimu wa kilimo kuanza ambapo ameagiza zoezi la kuzipeleka  walipo wakulima kote nchini lianze mara moja.

Bashe ametoa agizo hilo leo Oktoba 5, 2022 wakati akikagua mabanda yenye pembejeo za kilimo kabla ya kuzindua msimu wa kilimo wa 2022/ 2023 kwa Mkoa wa Singida ambayo pia aliongoza zoezi la ugawaji wa mbegu za alizeti zenye ruzuku ya Serikali.

Bashe alisikitika kusikia kuwa wakulima wa Mkoa wa Singida mpaka sawa hawajui watapata wapi mbolea maelezo yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi  (CCM) Mkoa wa Singida Juma Killimbah.

" Meh.Waziri kumekuwa na changamotochangamoto kubwa ya namna ya wakulima wetu kupata mbolea zaidi ya kusikia kwenye vyombo cha habari" alisem Killimbah.

Kufuatia maelezo hayo Waziri Bashe alimuita Afisa Kilimo wa Manispaa ya Singida na kumuhoji kuhusu jambo hilo licha ya kupatiwa mafunzo ya mfumo wa usambaziji wa pembejeo.

"Afisa kilimo baada ya kupewa mafuzo mmeweza kuyatoa kwa wananchi na madiwani ili mfumo huu wauelewe? Afisa kilimo alijibu hawajayatoa ndipo Waziri Bashe alikuwa mbogo na kusema mafunzo hayo waliyapata ili iweje kama si kuwafikishia walengwa".

Bashe alisema kuanza sasa hatapenda kusikia kuna Mkoa wakulima hawajapata mbolea hivyo aliagiza ipelekwe na kusambazwa maeneo yote na akawataka wakulima wajisajili kwa ajili ya kununua mbolea hiyo na ambaye hata jisajili hata kuweza kununua.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba akizungumza wakati akimkaribisha Waziri Bashe ili kuzindua msimu huo wa Kilimo wa 2022/ 2023 aliipongeza Serikali chini ya  Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza bajeti ya kilimo kutoka Sh.294.1 Bilioni hadi Sh.751.1 Bilioni  sawa na ongezeko la asilimia 155.34. bajeti  ambayo haijawai kutokea katika awamu zote za marais waliomtangulia.

Alisema lengo la Rais Samia kuongeza bajeti hiyo ni kuwatoa wananchi katika umaskini kwa kufanya kilimo cha Sayansi na si vinginevyo.

Alisema Mkoa wa Singida umejipanga kuongeza maeneo ya kilimo ambapo aliwahimiza wananchi kwenda mashambani kulima kwa bidii. 

Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Dk.Godfrey Mkamilo alisema katika suala la upatikanaji wa mbegu watashirikiana na ASA na kuhakikisha wanazalisha mbegu la zao la kimkakati la Alizeti.

Dk. Mkamilo pia alisema watasaidia kutoa mafunzo kwa maafisa ugani na wakulima kwa lengo la kuongeza tija na uzalishaji wa zao la alizeti hapa nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages

undefined

Contact Form

Name

Email *

Message *