Naibu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Singida, Petro Horombe akizungumza Machi 9, 2026 wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari ya robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/ 2026.
............................
Na Dotto Mwaibale, Singida
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa
Singida kwa kushirikiana na wadau imefanikiwa kurejesha magari manne yaliyokuwa
yakimilikiwa na Shirika lisilo la kiserikali la Sustainable Environment
Management Action (SEMA) lililopo mkoani Singida.
Magari hayo yalikamatwa na kampuni moja ya udalali kufuatia
shirika hilo kushindwa kulipa deni lililopelekea
magari hayo kukamatwa na kampuni hiyo ya udalali na kuyauza kinyume cha sheria.
Pamoja na magari hayo kwa mujibu wa Sheria ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa Sura ya 329 narejeo ya mwaka 2023 TAKUKURU Mkoa wa Singida imefanikiwa
kurejesha kiasi cha fedha zaidi ya Sh. Milioni 119.
Hayo yamebainishwa Machi 9, 2026 na Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida Petro
Horombe wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari ya robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/ 2026.
Horombe aliyataja magari hayo kuwa ni Isuzu Tiper lenye namba za usajili T 423 AED, Landlover
110 lenye namba T412 AED, Isuzu Tiper namba T 418 AED la kubebea vitu vizito
pamoja na Landcruizer VX yenye naamba za usajili 465 AED.
Akizungumzia utekelezajı wa ma}ukumu ya TAKUKURU, Horombe alisema taasisi hiyo imefanıkiwa kusaidia kurejesha
zaidi ya Sh. 119 milioni pamoja na magari manne
kutokana na kazi za uchunguzi.
“ Chambuzi za mifumo na ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo 25 yenye thamani ya Sh. 5,177,915,609.00 katika sekta za Elimu, Maji, Barabara, Afya, na Utawala kiasi hicho cha fedha kilirejeshwa,” alisema Horombe.
Akifafanua zaidi alisema kiasi cha Sh. S7,585,OOO.00 zilirejeshwa serikalini
kutokana na chunguzi za tuhuma mbalimbali za ubadhilifu wa mali za umma, na
magari manne baada ya uchunguzi kwa Taasisi miliki, kutokana na kuuzwa kinyume cha taratibu.
Horombe aliongeza kuwa Sh. 43,810,000.00 zililipwa kwa
wazabuni kwa ajili ya kusambaza vifaa vya ujenzi lakini vifaa hivyo
havikufikishwa kwenye maeneo ya miradi na baada ya ufuatiliaji, vifaa vyenye
thamani hiyo viliwasilishwa kwenye miradi husika.
Aidha, Horombe alisema
Mfanyabiashara wa vifaa vya
ujenzi alijipatia isivyostahili Sh.7,531,215.00 za
kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwa kutoa Stakabadhi ya kughushi ya EFD baada
ya kupokea malipo ya vifaa alivyosambaza kwenye utekelezaji wa mradi wa
maendeleo na baada ya ufuatiliaaji, mzabuni huyo aliwasilisha stakabadhi halali
ikiwa na makato hayo ya kodi.
Horombe akitoa ufafanuzi zaidi alisema Sh. 2,337,000.00
zililipwa kwa mzabuni baada ya kusambaza vifaa vya ujenzi katika utekelezaji wa
mradi visivyo na ubora na sifa zilizotajwa kwenye mkataba na baada ya
ufuatiliaji, mzabuni aliwasilisha vifaa stahiki kwa mujibu wa mkataba.
Fedha nyingine zilizorudishwa ni Sh. 2,009,884.63 za ushuru
wa huduma zilichukuliwa na wazabuni waliosambaza vłfaa vya ujenzi kwenye miradi
ya maendeleo isivyostahili baada ya kutokatwa kwenye malipo yao ambazo
zimerejeshwa kwenye akaunti za Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri baada ya
uchunguzi.
Alisema Sh.
1,563,625.25 za kodi ya zuio zilikatwa kwenye malipo ya wazabuni waliosambaza
vifaa vya ujenzi katika miradi mbalimbali ya maendeleo pasipo kuwasilishwa
kwenye mamlaka ya Napato Tanzania (TRA) na baada ya ufuatiliaji, fedha hizo
ziliwasilishwa TRA kwa mujibu wa sheria.
Horombe aliongeza kuwa Sh. 648,O0O.00 zililipwa ısivyo
halali kwa wazabuni waliosambaza vifaa vya ujenzi katika miradi ya maendeleo
kwa kuweka gharama kubwa ya vifaa kuliko bei halisi ya soko ambazo zimerejeshwa
kwenye akauntı za miradi husika.
Alitaja fedha nyingine zilizorejeshwa ni Sh. 43,810,000.00 ambazo zililipwa kwa wazabuni
kwa ajili ya kusambaza vifaa vya ujenzi lakini vifaa hivyo havikufikishwa
kwenye maeneo ya miradi naa baada ya ufuatiliaji, vifaa vyenye thamani hiyo
viliwasilishwa kwenye miradi husika.
Wakati huo huo Horombe alisema kuwa kupitia uchambuzi wa
mfumo wa vyombo vya watumia maji wameweza kurejesha Sh. 3,000,000.00 kwa
mwananchi mmoja ambaye alilipa kiasi hicho cha fedha kimakosa kwenye akaunti ya
jumuiya ya watumia maji ambapo awali uongozi wa jumuiya hiyo haukuwa tayari kurejesha
fedha hizo hadi TAKUKURU ilipoingilia kati.Skauti wakiwa kwenye mkutano huo. Wa kwanza kulia ni Kamishna wa Skaauti Wilaya ya Singida Veronica Mwambije.
Maafisa Usafirishaji wa Mkoa wa Singida wakiwa kwenye mkutano huo. Kutoka kushoto ni Mary Kalambo, Mwenyekiti wa madereva na wamiliki wa Bajaji na bodaboda Mkoa wa Singida, Abdul Swalehe na Katibu wa umoja huo Mkoa wa Singida, Abiud Mlowezi.

0 Comments